VYUO VYETU TANZANIA

VyuoVyetu Tanzania





Tuesday, February 19, 2013

ROSE MIGIRO ATEULIWA KUWA MKUU WA CHUO KIKUU HURIA CHA TANZANIA

ROSE MIGIRO ATEULIWA KUWA MKUU WA CHUO KIKUU HURIA CHA TANZANIA.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemteua Dkt. Asha Rose Migiro kuwa Mkuu wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania.

Taarifa iliyotolewa Dare Es Salaam na kutiwa saini , Jumatano, Januari 30, 2013 na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Y. Sefue imesema kuwa uteuzi huo ulianza Alhamisi ya Januari 17, mwaka huu wa 2013.

Mheshimiwa Asha Rose Migiro ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya Chama cha Mapinduzi (CCM) na Katibu wa NEC wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.

Aidha, Dkt. Migiro amepata kuwa Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN) na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wa Tanzania.

Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
IKULU
DAR ES SALAAM
30 Januari, 2013

source Aranse blog

Monday, January 14, 2013

KAMANDA KOVA azungumza na Wanafunzi wa IFM

                    Wanafunzi Baada ya kufika Wizara ya Mambo ya ndani  wakimsubiri RPC
 Rais wa serikali ya wanafunzi wa IFM  Michael S.Charse akijaribu kumuelewesha kamanda  KOVA kero inayo wakumba wanafunzi wa Ifm waishio kigamboni.
 Afande KOVA akizungumza na wanafunzi wa IFM pamoja na vyombo vya habari.


Wanafunzi wakielekea kigamboniii woteee kwa nguvu mojaaa tumechoka tumechoka

IFM...YALALAMIKIA UONGOZI JUU YA YANAYOTOKEA KIGAMBONI

 Wanafunzi wa IFM walipo kutana kwa pamoja katika viwanja vya chuoni hapo kabla ya kufikia uamuzi wa kwenda wizara ya mambo ya Mambo ya Ndani.Kupata hitimisho la matatizo ya ujambazi yanayotokea kigamboni kwa wanafunzi hoa, ambapo huibiwa laptop,simu na baadhi ya vitu vyenye thamani. Majambazi/wezi hao huja wengi takribani wanne na mapanga na visu na kuwaacha wanafunzi na majeraha, hali hiyo imekuwa tatizo zaidi kwa muda wa takribani wiki 4 bila chochote kufanyika mpaka imefikia  hatua ya wanafunzi wa kiume kuingiliwa kinyume na maumbilee

Baadhi yaWanafunzi wa IFM wakijaribu kuwasiliana na wanafunzi wenzao kuhusiana na matatizo yaliyotokea

Wednesday, December 12, 2012

JOBS KWA WALIO MALIZA CHUO NA VIGEZO

other jobs

Thursday, November 8, 2012

VYUONI KWETU UKOO

tutafika kweliiiii?mwanao/ndugu/rafiki wa kike akishindwa chuo kwa maana akidisco...usijudge mojakwa moja kuwa hasomi kuna mengi kama hayo uya onayooo katika picha....HAKI ELIMU..?

Sunday, October 28, 2012

TUMUOMBEE MTOTO HUYU..JULIANA MWINUKA

JULIA HUYU HAPA siku YA JUMATATUU ALIFANYIWA OPARESHENI CCBRT

Mtoto  Juliana Mwinuka
 
Majeraha  yaliyotokana na kuungua moto klatika  uso wa mtoto  mtoto  Juliana Mwinuka (16) mkazi  wa kitongoji cha Ushindi kata ya Mavanga  wilaya ya  Ludewa  mkoa  wa Njombe yameanza kuziba taratibu huku leo anategemea  kukutana na madaktari bingwa duniani ambao  wamewasili katika Hospitali ya CCBRT .

Kila mmoja  wetu tunaomba aendelee  kumwomba Mwenyezi Mungu kwa  dini yake ili kuweza  kutenda miujiza  ili mtoto  huyo aweze kupona.

 Mtandao huu unaendelea kuwapongeza wote wanaoendelea kuguswa na kuungana na wadau wengine kumchangia fedha za matibabu ,mtoto Juliana kama anavyoonekana akiwa ameunga uso wake kwa moto ni yatima anahitaji msaada wako ili kunusuru maisha yake waweza kutuma mchango wako kwa njia ya M-PESA katika namba hii 0754 026 299 au Tigo Pesa 0712 750199 namba hizi ni za mmiliki wa Bw Francis Godwin

Nawaomba tuungane kufanikisha kuokoa maisha ya mtoto Juliana Mwinuka na Mungu atatuongezea zaidi

Thursday, October 25, 2012

Waliogomea Shahada za UCLAS sasa kutunukiwa na UDSM


Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) kitakuwa na mahafali ya 42 tarehe 27 Oktoba 2012 na Novemba 3, 3012.

 Jumla ya wahitimu 3,643 watatunukiwa shahada na stashahada wakati wahitimu 902 wa Chuo Kikuu Kishiriki cha Ardhi (UCLAS) watatunukiwa shahada.

UCLAS kwa sasa ni sehemu ya UDSM.

Hayo yalisemwa na Makamu Mkuu wa wa UDSM, Profesa Rwekaza Mukandala akitoa taarifa kwa umma kupitia waandishi wa habari.

“Tunapenda kuufahamisha umma pia kuwa, katika mahafali ya sasa wanafunzi wa UCLAS na wao watatunukiwa shahada kama wanafunzi wa UDSM, uamuzi huu umefuatia kumalizika kwa kesi Lello & Others Vs Ardhi University, University of Dar es Salaam and Attornry General, Misc.Civil Cause No. 69 of 2008, iliyofunguliwa na wanafunzi wa UCLAS wakipinga kupata shahada za UCLAS kwa madai kuwa udahili wao ulibaki wa UDSM, hivyo UDSM kinakubalina kwa dhati na uamuzi wa Mahakama Kuu,” alisema Prof Mukandala.

UDSM imekubali kuwatunuku shahada mbalimbali wahitimu hao 902 waliomaliza masomo yao UCLAS ambao awali waligoma kutunukiwa shahada zao na chuo hicho (UCLAS) katika Mahafali ya 42 kutokana na madai kuwa walipata udahili chini ya UDSM wakati UCLAS kilipopata hadhi ya kuwa chuo kikuu kinachojitegemea mwaka 2007 hivyo walistahili kutunukiwa shahada na chuo kilichowadahili. Wanafunzi hao ni wale waliohitimu masomo katika miaka ya 2007 hadi 2010.

Wanafunzi hao kwa kupinga suala hilo walifungua kesi mahakamani dhidi ya Chuo Kikuu cha Ardhi, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

“Sisi Chuo Kikuu cha Dar es Salaam tumekubaliana kwa dhati na uamuzi huu wa mahakama na tumeamua kuwatunuku shahada wanafunzi hao kwa vile hakuna rufaa iliyokatwa dhidi ya uamuzi huo,” alisema Profesa Mukandala.

Kati ya watakaotunukiwa shahada mbalimbali, 28 watatunukiwa Shahada za Uzamivu, 671 Shahada ya Uzamili; 153 Stashahada za Uzamili na 2, 790 Shahada ya Kwanza.

Licha ya mahafali hayo, Profesa Mukandala alisema chuo hicho kitahitimisha maadhimisho ya miaka 50 ya kuanzishwa kwake kwa kufanya shughuli mbalimbali ikiwamo kufanya mkutano na wahitimu waliowahi kusoma chuoni hapo shughuli ambayo itafanyika Alhamisi.

Profesa Mukandala alisema wakati wa kuhitimisha sherehe hizo, shughuli zitakazofanyika ni kuweka jiwe la msingi la jengo la kituo cha wanafunzi, kuzindua Dira ya Chuo hicho (UDSM Vision 2061) na kutoa tuzo mbalimbali kwa watu na vikundi vilivyotoa mchango uliotukuka kwa chuo kikuu katika miaka 50 iliyopita.

Akizungumzia dira hiyo, alisema itakuwa ni ya nusu karne ijayo na malengo yake ni kufikia mwaka 2061 chuo kitakuwa katika nafasi za juu za viwango vya ubora vya kimataifa.

---
Habari via Nipashe  na DHabariLeo

Wednesday, October 24, 2012

MKUTANO WA KWANZA WA UMOJA WA VYUO VIKUU ELIMU YA JUU VYA AFRIKA MASHARIKI

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akihutubia wakati akifungua mkutano wa kwanza wa Umoja wa Vyuo Vikuu  unaoshirikisha pia Kamisheni ya Biashara ya Afrika Mashariki. Mkutano huo unafanyika kwa siku tatu jijini Arusha na unajumuisha wakuu na wawakilishi wa vyuo mbalimbali vya elimu ya juu katika ukanda wa Afrika Mashariki.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiteta jambo na Mwenyekiti wa Umoja wa Mawaziri wa Afrika Mashariki, Musa Sirima, wakati wa uzinduzi wa mkutano wa kwanza wa Umoja wa Vyuo Vikuu  unaoshirikisha pia Kamisheni ya Biashara ya Afrika Mashariki. Mkutano huo unafanyika kwa siku tatu jijini Arusha na unajumuisha wakuu na wawakilishi wa vyuo mbalimbali vya elimu ya juu katika ukanda wa Afrika Mashariki.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisikiliza maelezo kutoka kwa Makamu Mkuu wa Chuo cha Mtakatifu Augustine, Dkt. Charles Kitima, wakati alipokuwa akitembelea kukagua mabanda ya maonyesho baada ya kufungua mkutano wa kwanza wa Umoja wa Vyuo Vikuu  unaoshirikisha pia Kamisheni ya Biashara ya Afrika Mashariki. Mkutano huo unafanyika kwa siku tatu jijini Arusha na unajumuisha wakuu na wawakilishi wa vyuo mbalimbali vya elimu ya juu katika ukanda wa Afrika Mashariki.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa mkutano wa kwanza wa Umoja wa Vyuo Vikuu  unaoshirikisha pia Kamisheni ya Biashara ya Afrika Mashariki. Mkutano huo unafanyika kwa siku tatu jijini Arusha na unajumuisha wakuu na wawakilishi wa vyuo mbalimbali vya elimu ya juu katika ukanda wa Afrika Mashariki. Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais

KILUVYA

KILUVYA
MASHONO

UDOM

UDOM
DODOMA UNIVERSITY